sw_tn/psa/072/018.md

1018 B

Taarifa ya Jumla:

Mistari hii ni zaidi ya mwisho wa zaburi hii. Ni kauli ya kufunga ya kitabu kizima cha 2 cha Zaburi, kinachoaanza Zaburi 42 hadi Zaburi 72.

Yahwe Mungu, Mungu wa Israeli, abarikiwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Watu wambariki Yahwe Mungu, Mungu wa Israeli"

Jina lake tukufu libarikiwe milele

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Watu walibariki jina lake tukufu milele" au kufanya "jina" kama namna nyingine ya kusema Yahwe mwenyewe, "watu daima wajue jinsi alivyo mtukufu"

Jina lake tukufu libarikiwe

"yeye aliye mtukufu, abarikiwe"

dunia nzima ijazwe na utukufu wake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "utukufu wake uijaze dunia yote" au "aijaze dunia yote na utukufu wake"

Amina na Amina

Neno "Amina" linarudiwa kusisitiza kukubali kilichosemwa. "Hakika iwe hivyo"

Maombi ya Daudi mwana wa Yese yanaisha

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Daudi mwana wa Yese amemaliza maombi yake" au "Haya ni maombi ya mwisho ya Daudi mwana wa Yese"