1.3 KiB
Taarifa ya jumla.
Neno "ninyi" linamaanisha waamini waliotawanyika ambao Yakobo anawaandikia.
Sogeeni karibu na Mungu, na yeye atakaribia karibu nanyi
Hapa anamaanisha kuwa wakweli na wazi kwa Mungu.
Safisheni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na takaseni mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.
Hizi ni sentensi mbili zinazoendana.
Safisheni mikono yenu
Hii ni amri kwa watu kufanya mambo ya haki na sio maovu. "Ishini namna ambavyo inampendeza Mungu"
Takaseni mioyo yenu
"mioyo" inamaanisha mawazo ya mtu na hisia zake" Mheshimu Mungu kwa mawazo yako"
nia mbili
"Nia mbili" linamaanisha mtu ambaye hawezi kufanya maamuzi juu ya jambo fulani. "Mtu ambaye hawezi kuamua amtii Mungu au la"
Huzunika, omboleza, na Lia
Maneno haya matatu yana maana moja. Yakobo anayatumia kwa pamoja kuonesha kuwa watu watahuzunika sana kwa kutokumtii Mungu" Yakobo anasema haya kama amri.
Geuzeni kicheko chenu kuwa huzuni na furaha yenu kuwa maombolezo
Hapa kicheko kimezungumzwa kuwa kitageizwa kuwa huzuni na furaha kuwa maombolezo. "Acheni kucheka na mtubu kwa Mungu"
Nyeyekeeni wenyewe mbele za Bwana
"Jinyenyekezeni mbele za Mungu"
Atawainua juu
Yakobo anazungumza namna ambavyo Mungu anamuheshimu mtu mnyenyekevu na kumnyanyua toka chini. "atakuheshimu wewe"