forked from WA-Catalog/sw_tn
33 lines
1.1 KiB
Markdown
33 lines
1.1 KiB
Markdown
# Maelezo ya jumla
|
|
|
|
Katika mistari ya 34-37 Nebukadneza anaongelea katika nafsi ya kwanza katika kueleza jibu lake kwa Mungu.
|
|
|
|
# utimamu wa akili zangu uliponirudia
|
|
|
|
Mahali hapa utimamu unaongelewa kana kwamba ulikuwa na uwezo wa kurudi kwa nguvu zake.
|
|
|
|
# utukufu wangu na fahari yangu ilinirudia
|
|
|
|
Mahali hapa utukufu wake na fahari kwa pamoja unaongelewa kana kwamba ulikuwa na uwezo wa kurudi kwa nguvu zake .
|
|
|
|
# utukufu wangu na fahari yangu
|
|
|
|
Maneno haya yana maana sawa na yametumika kutilia mkazo juu ya ukubwa wa utukufu wake.
|
|
|
|
# watu wenye heshima walitafuta msaada wangu
|
|
|
|
"Watu wangu wa heshima waliomba msaada wangu tena"
|
|
|
|
# Nilirudishwa kwenye kiti changu cha enzi, na nilipewa ukuu zaidi
|
|
|
|
Mahali hapamaneno "kiti cha enzi" yanarejelea mamlaka yake ya kutawala. Pia muundo tendaji waweza kutumika. "Nilirudi kutawala ufalme wangu tena, na nilipata ukubwa zaidi."
|
|
|
|
# ninamsifu, ninamtukuza na kumheshimu
|
|
|
|
Maneno haya matatu kimsingi yana maana moja na yametumika kutia mkazo juu ya jinsi alivyomsifu Mungu.
|
|
|
|
# wanaotembea katika kiburi chao wenyewe.
|
|
|
|
Kitenzi "kutembea" kinamrejelea mtu anayetenda kwa kiburi.
|
|
|