sw_tn/act/15/intro.md

1.4 KiB

Matendo 15 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Tafsiri zingine zimeweka kila mstari wa ushairi mbele ya kulia kuliko maandishi mengine ili kurahisisha kusoma. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la Kale 15:16-17

Mkutano unaoelezwa na Luka katika sura hii huitwa "Baraza la Yerusalemu." Huu ulikuwa nimuda ambapo viongozi wengi wa kanisa walikuja pamoja kuamua iwapo waumini walihitaji kufuata sheria zote za Musa.

Dhana maalum katika sura hii

Ndugu

Katika sura hii, Luka anaanza kwa kutumia neno "ndugu" kumaanisha Wakristo wenzake badala ya Wayahudi wenzake.

Kutii sheria za Musa

Waumini wengine walitaka watu wa mataifa watahiriwe kwanza kwa vile Mungu alimuambia Abarahamu kwamba yeyote aliyetaka kuwa wake lazima angepashwa tohara na hii sheria ingedumu. Kwa upande mwingine Paulo na Barnaba walikuwa wameshuhudia Mungu akiwapa watu wa Mataifa kipaji cha Roho Mtakatifu na kwa hivyo hawakusisitiza watu wa mataifa watahiriwe. Makundi yote mawili yalienda Yerusalemu kwa uamuzi wa viongozi wa kanisa kuhusu swala hilo.

"Mjiepushe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongolewa, na uasherati."

Kuna uwezekano ya kwamba viongozi wa kanisa walitoa uamuzi kwa hizi sheria ili Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa waweze kuishi pamoja na kula chakula kimoja pamoja.

<< | >>