sw_tn/act/03/11.md

966 B

Sentensi unganishi

Baada ya kuponywa kwa mtu aliyekuwa hawezi kutembea, Petro anaongea na umati.

Maelezo ya jumla

Katika ukumbi uluokuwa ukiitwa Solomoni. Hapa iko wazi kuwa Petro alitumia eneo hili kutoa hotuba yake, haikuwa ndani ya hekalu ambamo ni makuhani tu walioruhusiwa kuingia.

maajabu makuu

"kujawa na mshangao" au "Kaduwaa"

Wakati Petro alipoona hiki

"Petro alipoona mkutano unaongezeka na kuzidi kushangaa.

Ninyi watu wa Israeli

"Waisraeli wenzangu". Petro akizungumza na mkutano. Neno "watu" katika mkutadha huu inahusisha kila mmoja aliyepo.

kwa nini mnashangaa?

Petro anauliza swali hili ili kuwaambia watu wasishanganzwe na kile kimetokea.

Kwa nini mnayaelekeza macho yenu kwetu, kama kwamba tumemfanya huyu atembee kwa nguvu zetu wenyewe au uchaji wetu?

Petro anawauliza swali hili ili kuwathibitishia kuwa tukio hilo halikutendwa na wao yaani Petro na Yohana, hivyov wasiwatazame wao kama ndiyo waliomponya yule kiwete.