forked from WA-Catalog/sw_tn
37 lines
1.2 KiB
Markdown
37 lines
1.2 KiB
Markdown
# Maelezo ya Jumla
|
|
|
|
Yahwe anaendelea kueleza ahadi zake kwa Mfalme Daudi kupitia nabii Nathani.
|
|
|
|
# Nitateua mahali
|
|
|
|
"Nitachagua sehemu"
|
|
|
|
# nitawapanda pale
|
|
|
|
Yahwe anawafanya watu waishi katika nchi daima na kwa usalama inazungumzwa kama kama angewapanda katika nchi.
|
|
|
|
# na hawatasumbuliwa tena
|
|
|
|
Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji: Yaani: "na hakuna atakayewasumbua tena"
|
|
|
|
# kutoka siku
|
|
|
|
Hapa "siku" inawakilisha kipindi kirefu.
|
|
|
|
# Niliwaamru waamzi
|
|
|
|
Baada ya Waisraeli kuingia katika nchi ya Kanaani na kabla ya kuwa na wafalme wa kuwatawala, Mungu aliteua viongozi walioitwa "waamzi" kuwaongoza katika nyakati za shida.
|
|
|
|
# Nami nitakupa pumziko kutoka kwa adui zako wote...anakwambia kwamba atakutengenezea nyumba
|
|
|
|
Yaweza kufasiriwa: "Nami nitampa pumziko kutoka kwa adui zake wote... anamwambia kwamba atamtengenezea nyumba"
|
|
|
|
# Nikupumzisha kutoka kwa adui zako wote
|
|
|
|
"Nitakupa usalama kutoka kwa adui zako wote." Hapa "pumziko" ni nomino dhahania. Yaweza kuwa: "Nitawafanya adui zako wote waache kukushambulia"
|
|
|
|
# Nitakutengenezea nyumba
|
|
|
|
Maana hii hapa ya "nyumba" inarejea kwa wazao wa Daudi kuendelea kumiliki katika Israeli. Katika 7:3 Yahwe alimuuliza Daudi ikiwa angemjengea nyumba. Pale "nyumba" inawakilisha hekalu.
|
|
|