sw_tn/1jn/03/01.md

1.0 KiB

Angalia ni pendo la namna gani ametupatia Baba.

"Fikiria kuhusu kiasi gani Baba yetu anavyotupenda sisi."

Sisi...Tu.

Katika 3:1-3 viwakilishi nomino hivi, humtaja Yohana, wasikilizaji wake, na waumini wote.

Lazima tuitwe watoto wa Mungu.

Hii inaweza kutafsiriwa kwa kitenzi tendaji: "Baba lazima atuite sisi watoto wake."

Watoto.

Hapa hii inamaanisha watu wa Mungu kwa imani katika Yesu.

Ulimwengu haututambui, kwa sababu hakumtambua Yeye.

Hapa "ulimwengu" humaanisha watu ambao hawamheshimu Mungu. Kile ambacho ulimwengu haukijui, hakiwezi kufanywa dhahili: Wale ambao hawamheshimu Mungu, hawajui kwamba sisi ni wa Mungu, kwa sababu hawakumjua Mungu.

Haijadhihirika bado.

Hii inaweza kutafsiriwa kwa kitenzi tendaji: "Mungu hajadhihirisha."

Na kila mtu ambaye ana ujasiri huu kuhusu wakati ujao ulioelekezwa kwake, hujitakasa mwenyewe kama yeye alivyo mtakatifu.

"Kila mtu ambaye anatarajia kwa ujasiri kumuona Kristo kama alivyo, ataendelea kujitakasa mwenyewe kwa sababu Kristo ni mtakatifu."