sw_tn/zec/10/04.md

697 B

Kutoka kwao litatoka jiwe kuu la pembeni

"Jiwe la pembeni litatoka kwao." Kiongozi mhimu anazungumzwa kama vile jiwe kuu la msingi wa jengo.

kutoka kwao kitatoka kigingi cha hema

"kigingi cha hema kitatoka kwao." Viongozi wakuu wanazungumzwa kama vile vigingi vikubwa vinavyolishikilia hema mahali pake.

kutoka kwao utatoka upinde wa vita

"upinde wa vita utatoka kwao." Viongozi wa kijeshi wanasemwa kama walikuwa upinde uliotumiwa vitani.

Watakuwa kama mashujaa

"Watakuwa wenye nguvu vitani"

wawakanyagao adui zao katika matope ya mitaani vitani

"wawashindao adui zao kwa ukamilifu"

nao watawaabisha wapanda farasi

"nao watawashinda adui zao wapiganao nao katika farasi"