sw_tn/zec/09/11.md

745 B

Lakini kwenu

Hapa "ninyi" inamaanisha watu wa Israeli.

shimo ambalo halina maji

Shimo hapa linawakilisha uhamisho.

Rudini ngomeni

"Rudini katika nchi yenu mahali mtakapokuwa salama"

wafungwa wa tumani

Hii inamaanisha Waisraeli waliokuwa kifungoni waliokuwa bado wanamatumaini kwamba Mungu atawakomboa.

pinda Yuda kama upinde wangu

Watu wa Yuda wanatajwa kama walikuwa upinde uliobebwa na Mungu kwa vita.

kulijaza podo langu kwa Efraimu

Watu wa Israeli, ufalme wa kaskazini, wanatajwa kama walikuwa mishale ambayo Mungu angewapigia adui zake. Podo ni mfuko unaotunza mishale ya askari.

Nimewainua wana wenu, Sayuni, kinyume cha wana wenu, Ugiriki,

Mungu anazungumza na watu wa mataifa mawili tofauti kwa wakati mmoja.