sw_tn/zec/09/09.md

1004 B

Piga kelele kwa furaha, ewe binti Sayuni! Piga kelele kwa shangwe, ewe binti Yerusalem!

Mistari hii miwili inamaanisha jambo moja na inazidisha agizo la kufurahi.

binti Sayuni... binti Yerusalem

"Sayuni" ndiyo "Yerusalemu." Nabii anauzungumzia mji kanakwamba ni binti.

juu ya punda, juu ya mwanapunda

Vifungu hivi viwili kimsingi vinamaanisa jambo moja na vinamrejerea mnyama mmoja. Mstari wa pili unaweka wazi kwamba huyu ni mwanapunda.

kukatilia mbali kibandawazi kutoka Efraimu

"Kuharibu vibandawazi vitumikavyo kwa vita katika Israeli"

farasi kutoka Yerusalemu

"farasi wa vita katika Yerusalemu"

upinda utakatiliwa mbali kutoka katika vita

Hapa upinde unawakilisha silaha zote zitumikazo kwa vita. "Silaha zote za vita zitateketezwa"

Maana atanena amani kwa mataifa

Hapa tendeo la kutangaza amani linawakilisha tendo la kufanya amani.

utawala wake utakuwa kutoka bahari hata bahari, na kutoka katika mto hadi miisho ya dunia

"ufalme wake utakuwa juu ya dunia yote!"