sw_tn/rev/16/17.md

1.0 KiB

Kauli Unganishi:

Malaika wa saba amwaga bakuli la saba la ghadhabu ya Mungu.

alimwaga kutoka kwenye bakuli lake

Neno "bakuli" linamaanisha kile kilichomo. "kumwagwa divai kutoka katika bakuli lake" au " kumwaga ghadhabu ya Mungu kutoka katika bakuli lake"

Kisha sauti kuu ikasikika kutoka hekaluni na kutoka kwenye kiti cha enzi

Hii inamaanisha mtu aliyekuwa kwenye kiti cha enzi au karibu na kiti cha enzi alinena kwa sauti ku. Haiko wazi ni nani anayezungumza.

miale ya mwanga wa radi

Mwanga unaotokea wakati radi ikipiga.

ngurumo, vishindo vya radi

Hii ni miungurumo ya sauti ambayo radi husababisha.

Mji mkuu uligawanyika

"Tetemeko liliugawanya mji mkuu"

Kisha Mungu akakumbuka

"Kisha Mungu akawazia" au "Kisha Mungu akaanza kuwa makini na." Hii haimaanishi kuwa Mungu alikumbuka jambo alilosahau.

akaupa mji huo kikombe kilichokuwa kimejaa divai kutoka kwenye ghadhabu yake iliyo kali

Divai ni isharaya ya ghadhabu yake. Kuwafanya watu kuinywa ni ishara ya kuwaadhibu. "aliwafanya watu wa mji huo kunywa divai inayoashiria ghadhabu yake"