sw_tn/rev/12/10.md

1015 B

"nikasikia"

anayezungumza ni Yohana.

nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni

Neno "sauti" inaonesha mtu anayezungumza. "Nikasikia mtu akinena kwa sauti toka mbinguni"

sasa wokovu umekuja, nguvu

Mungu kuwaokoa watu kwa nguvu zake inazungumziwa kana kwamba wokovu wake na nguvu zake ni vitu vinavyoweza kuja. "Sasa Mungu amewaokoa watu wake kwa nguvu zake"

umekuja

"kuanza kuwepo kabisa" au "kutokea" au "kuwa kweli." Sio kwamba vitu hivi havikuwepo kabala, lakini sasa Mungu anavidhihirisha kwa sababu wakati wake kutokea "umekuja."

ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake

Utawala wa Mungu na mamlaka ya Kristo yanazungumziwa kama vile vinakuja. "Mungu atawala kama mfalme, na Kristo wake anamamlaka yote"

mshitaki wa ndugu zetu ametupwa chini

Huyu ni joka aliyetupwa chini katika 12:10

ndugu zetu

Waumini wenzao wanazungumziwa kana kwamba walikuwa ni ndugu. "waumini wenzetu"

mchana na usiku

Hizi sehemu mbili za siku zinatumika pamoja kumaanisha "wakati wote" au "bila kukoma"