sw_tn/rev/05/01.md

738 B

Kauli unganishi:

Yohana anaendelea kueleza alichokiona katika maono ya kiti cha enzi cha Mungu.

Kisha nikaona

"Baada ya kuona hivyo vitu ,nikaona"

yule aliyekuwa amekaa katika kiti cha enzi

Hii ni sawa sawa na "moja" kama 4:1

gombo lililoandikwa mbele na nyuma

"gombo linye maandishi mbele na nyuma"

lilikuwa limetiwa mihuri saba

"lilikuwa limefungwa na mihuri saba"

Nani astahiliye kulifungua gombo na kuzivunja mihuri yake?

Mtu huyu atahitaji kuivunja mihuri ili kuifungua gombo. "Nani anayestahili kuvunja mihuri na kufungua gombo?"

Nani astahiliye kulifungua gombo na kuzivunja mihuri yake?

Hii inaweza kutafsiriwa kama amri. "Acha yule ambaye anastahili kufanya hivi aje avunje mihuri na kuifungua gombo!"