sw_tn/rev/01/09.md

1018 B

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaeleza jinsi maono yake yalivyoanza na maelekezo aliyopewa na Roho.

yenu...nanyi

Hii humaanisha waumini katika makanisa saba

anayeshiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na uvumilivu thabiti ulio katika Yesu

"aliye na fungu katika ufalme wa Mungu. Ninateseka pia na kuvimilia majaribu pamoja nanyi kwa sababu sisi ni mali ya Yesu"

kwa sababu ya neno la Mungu

"kwa sababu niliwaambia wengine kuhusu neno la Mungu"

katika Roho

Yohana anazungumzia kuvutwa na Roho ya Mungu kana kwamba alikua katika Roho. "kushawishika na Roho" au "Roho alinishawishi"

siku ya Bwana

siku ya kuabudu kwa waumini wa Kristo

sauti ya juu kama ya tarumbeta

Sauti ilikua na sauti kuu sana ikafanana na tarumbeta

tarumbeta

Hii humaanisha chombo cha kutengeneza muziki au kuwaita watu kwa ajili ya tangazo au mkutano.

kwenda Smirna, kwenda Pergamo, kwenda Thiatira, kwenda Sardi, kwenda Philadelphia, na kwenda Laodikia

Haya ni majina ya miji uliko Asia ambayo ni Uturuki ya leo