forked from WA-Catalog/sw_tn
28 lines
970 B
Markdown
28 lines
970 B
Markdown
# Taarifa ya Jumla:
|
|
|
|
Mwandishi anachukulia kuwa msomaji anafahamu historia ya jinsi Daudi alivyochaguliwa kuwa mfalme.
|
|
|
|
# Nimeweka taji kwa aliye hodari
|
|
|
|
Kuweka taji juu ya kichwa cha mtu ni ishara ya kumfanya kuwa mfalme. "Nimemfanya mtu hodari kuwa mfalme"
|
|
|
|
# Nimeweka taji kwa aliye hodari
|
|
|
|
Tafsiri zingine za Biblia zina "kumpa nguvu aliye hodari" au "kumsaidia aliye hodari."
|
|
|
|
# Nimemwinua mmoja niliyemchagua miongoni mwa watu
|
|
|
|
Hapa "nimemwinua" inamaanisha kuchagua. Inadokezwa kuwa Mungu alimchagua mtu huyu kuwa mfalme. "Nimemchagua mmoja miongoni mwa watu kuwa mfalme"
|
|
|
|
# kwa mafuta yangu matakatifu nimempaka
|
|
|
|
Hapa kumwaga mafuta juu ya kichwa cha mtu ni ishara kuwa Mungu anamchagua huyo mtu kuwa mfalme.
|
|
|
|
# Mkono wangu utamshika; mkono wangu utamtia nguvu
|
|
|
|
Hapa "mkono" unamaanisha nguvu na mamlaka ya Yahwe. "nitamshika na kumfanya kuwa na nguvu"
|
|
|
|
# mwana wa uovu
|
|
|
|
Mwandishi anawazungumzia wale wenye sifa au tabia ya uovu kama "wana wa uovu." "mtu mwovu"
|