1.1 KiB
wanaokutafuta
Kumtafuta Mungu inaashiria kati ya 1)kumwomba Mungumsaada au 2) kumwaza Mungu na kumtii. "kukuomba msaada" au"kukuwaza na kukutii"
washereheke na kufurahi
Misemo hii miwili inamaana sawa na inasisitiza uzito wa furaha. "kufurahi sana" au "kuwa na furaha sana"
wanaopenda waokovu wako
Nomino dhahania ya "wokovu" inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wanaokupenda kwa sababu umewaokoa"
daima waseme
Hapa ni kukuza kwa neno ili kusisitiza umihimu wa kumsifu Mungu mara kwa mara.
Mungu asifiwe
Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Acha kila mtu amsifu Mungu"
maskini na mhitaji
Hapa maneno "maskini" na "mhitaji" yanamaana ya kufanana na yanasisitiza kuwahakuweza kujihudumia mwenyewe. "mhitaji sana"
harakisha kwangu
Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba anamkimbilia mwandishi ili amsaidie. "njoo upesi unisaidie!"
wewe ni msaada wangu na unaniokoa
Hapa msemo "unaniokoa" unaeleza jinsi Mungu alivyo msaada wake. "unanisaidia kwa kuniokoa"
usichelewe
Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "tafadhali njoo upesi"