sw_tn/psa/039/001.md

28 lines
729 B
Markdown

# Taarifa ya Jumla:
Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.
# Kwa mwanamuziki mkuu
"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"
# Yeduthuni
Mmoja wa wanamuziki wakuu wa Daudi alikuwa na jina hili. Hii inaweza kumaanisha ni yeye.
# Zaburi ya Daudi
Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.
# Nitachunga ninachozungumza
"Nitakuwa msikivu katika vitu nitakavyosema"
# ili nisitende dhambi kwa ulimi wangu
Hapa "ulimi" inamaanisha maneno ya mwandishi. "ili nisizungumze maneno mabaya dhidi ya Yahwe"
# nitajitia lijamu
Hii inamaanisha kufunga mdomo. Hapa Daudi anamaanisha kuwa hatazungumza akiwa na mtu mwovu.