sw_tn/psa/037/022.md

1.1 KiB

Wale walio barikiwa na Mungu

"Wale ambao Mungu anawabariki"

watarithi nchi

Umiliki wa nchi unazungumziwa kanakwamba umepokelewa kama urithi. "watapokea nchi kama mali yao" au "wataruhusiwa kuishi kwa usalama katika nchi"

wale waliolaaniwa naye

"wale ambao Yahwe amewalaani"

watakatwa

Uharibifu wa watu waovu unazungumziwa kana kwamba ni tawi la mmea uliokatwa na kutupwa.

Ni kupitia Yahwe hatua za mtu zinaimarishwa ... inpendeza machoni pa Mungu

"Kama mtu anaishi katika njia ya kupendeza machono pa Yahwe, Yahwe ataimarisha njia zake"

Ni kupitia Yahwe hatua za mtu zinaimarishwa

"Yahwe ndiye anayemwezesha mtu kufanikiwa"

mtu ... mtu

Hii haimaanishi mtu bayana, lakini kwa watu kwa ujumla.

hatua za mtu

Hatua zinawakilisha jinsi mtu anavyoishi. "jinsi mtu anavyoishi"

Ingawa anajikwaa, hataanguka

Hapa "kujikwaa" na "kuanguka" inamaanisha jinsi mtu anavyojibu katika vipindi vigumu. "Ingawa ana vipindi vigumu, hatashindwa kabisa"

anamshika kwa mkono wake

Hapa "mkono wake" inamaanisha nguvu ya Yahwe, na "kumshika" inamaanisha kumlinda. "kumlinda na nguvu yake"