sw_tn/psa/037/011.md

709 B

wapole

Hii inamaanisha watu walio wapole. "watu wapole"

watarithi nchi

Kumiliki nchi kunazungumziwa kana kwamba itapokelewa kama urithi. "watapokea nchi kama urithi wao" au "wataishi kwa usalama katika nchi"

mtu mwovu

Hii haimaanishi mtu bayana. Inamaanisha watu waovu kwa ujumla. "mtu mwovu"

mwenye haki

Hii haimaanishi mtu bayana. Inamaanisha watu wenye haki kwa ujumla. "mtu mwenye haki"

kusaga meno

Mtu mwovu anamchukia mtu mwenye haki sana hadi anasaga meno yake pamoja kuonesha hasira yake.

siku yake inakuja

Inadokezwa kuwa "siku yake" itakuwa siku ya hukumu. "siku inakuja ambapo Yahwe atamhukumu na kumwadhibu" au "siku inakuja ambapo Yahwe atamhukumu na kumwadhibu mtu mwovu"