sw_tn/psa/027/007.md

727 B

Sikia, Yahwe, sauti yangu

Hapa "sauti" inamaanisha kuwa mwandishi anasema. "Nisikie, Yahwe"

nijibu

Hii inaashiria kuwa Yahwe anasikia maombi ya mwandishi na Yahwe atafanya kile mwandishi anachoomba. "jibu ombi langu" au "fanya ninachokuomba"

Moyo wangu unasema

Hapa "moyo" unawakilisha akili na mawazo ya mtu. "Moyoni mwangu nasema" au "Ninajiambia"

Utafute uso wake

Mtu kwenda hekaluni kumwomba Yahwe inazungumziwa kana kwamba mtu huyo anamtafuta Yahwe. "Hapa "uso" unamwakilisha Mungu. "Nenda ukaombe kwa Yahwe"

Nautafuta uso wako, Yahwe

Mtu kwenda hekaluni kumwomba Yahwe inazungumziwa kana kwamba mtu huyo anamtafuta Yahwe. "Hapa "uso" unamwakilisha Mungu. "Nitakuja kwenye hekalu lako na kuomba kwako"