sw_tn/psa/018/035.md

692 B

ngao ya wokovu wako

Hapa mwandishi anazungumzia ulinzi wa Mungu kana kwamba ni ngao. Nomino dhahania ya "wokovu" inaweza kuelezwa kama kitenzi "okoa." "ulinzi wako na kuniokoa"

Mkono wako wa kuume ... fadhili zako

Zote hizi ni njia zingine za kumwakilisha Mungu mwenyewe.

sehemu pana kwa ajili ya miguu yangu chini yangu

Mwandishi anazungumzia ulinzi ambao Mungu ameutoa kana kwamba ni eneo pana kwa ajili yake kusimama. "sehemu salama kwa ajili yangu"

miguu yangu haijateleza

Hapa "miguu yangu" inamaanisha mtu mwenyewe. Mwandishi anazungumzia usalama wa ulinzi wa Mungu kana kwamba alikuwa akisimama mahali ambapo hawezi kuteleza wala kuanguka. "Sijateleza" au "Niko salama"