sw_tn/psa/018/004.md

580 B

Kamba za mauti zinanizunguka

Daudi anazungumzia kifo kana kwamba ni mtu anayeweza kukamata na kumfunga kwa kamba. "Nilikuwa nataka kuuwawa"

maji yanayokimbia ya yasiyofaa

Daudi ni mnyonge kana kwamba anabebwa na mafuriko ya maji yanayokimbia. "Nilihisi kuwa mnyonge kabisa"

Kamba za kuzimu zinanizunguka; mitego ya mauti imeninasa

Hapa "kuzimu," sehemu ya wafu, na "mauti" zinazungumziwa kana kwamba ni watu wanaoweza kumzunguka na kumtega. Vishazi hivi viwili vina maana ya kufanana na wazo linarudiwa kwa ajili ya mkazo. "Nilihisi kubanwa na nikadhani ninaenda kufa"