sw_tn/mrk/12/28.md

1019 B

Sentensi unganishi

Mwandishi anamuuliza Yesu swali la akili, ambalo Yesu analijibu.

Alimuuliza

"Mwandishi alimuuliza Yesu"

iliyo ya muhimu zaidi katika zote..iliyo ya muhimu ni hii

Taarifa inayokosekana inaweza kuongozwa. "amri iliyo ya muhimu zaidi katika zote...amri iliyo ya muhimu anasema"

Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu, Bwana ni mmoja.

"Sikiliza, Israeli! Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja"

kwa moyo wako yote, kwa roho yako yote

"Moyo" na "roho" ni mifano ya utu wa ndani na tamaa zake na hisia. "kwa chote unachotaka na kujisikia"

kwa akili yako yote, na kwa nguvu zako zote

"akili" urejea kwa namna mtu anavyofikiri na "nguvu" urejea kwa nguvu za mtu kufanya mambo. "kwa yote unayofikiri, na kwa yote unayofanya"

umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe

Yesu anatumia mfanano kulinganisha namna watu wanavyopaswa kupendana wao kwa wao kwa upendo ule ule kama wanavyojipenda wenyewe"

zaidi ya hizi

Hapa neno "hizi" urejea kwa amri mbili ambazo Yesu alikuwa amewambia watu.