sw_tn/mrk/11/intro.md

1.3 KiB

Marko 11 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi kwa upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB hufanya hivi kwa mashairi katika 11:9-10,17, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Punda na mwana-punda

Yesu aliingia Yerusalemu juu ya mnyama. Kwa njia hii alikuwa kama mfalme aliyeingia mjini baada ya kushinda vita muhimu. Pia, katika Agano la Kale, wafalme wa Israeli walikuwa wanapanda punda. Wafalme wengine walipanda farasi. Kwa hiyo Yesu alikuwa akionyesha kwamba alikuwa mfalme wa Israeli lakini hakukuwa kama wafalme wengine.

Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya tukio hili. Mathayo na Marko waliandika kwamba wanafunzi walimletea Yesu punda. Yohana aliandika kwamba Yesu alipata punda. Luka aliandika kwamba walimletea mwana-punda. Mathayo tu aliandika kwamba kulikuwa punda pamoja na mwana-punda. Hakuna anayejua hakika ikiwa Yesu alipanda punda au mwana-punda. Ni bora kutafsiri kila maneno haya kama yanoyoonekana katika ULB bila kujaribu kuwafanya wote wanasema jambo sawa. (Ona: Mathayo 21:1-7 na Marko 11:1-7 na Luka 19:29-36 na Yohana 12:14-15)

<< | >>