sw_tn/mrk/08/14.md

928 B

Sentensi unganishi

Wakati Yesu na wanafunzi wake wakiwa ndani ya mtumbwi, walikuwa na majadiliano kuhusu kuelewa kudogo kati ya Mafarisayo na Herode, ijapokuwa walikuwa wamekwisha ona ishara nyingi.

Sasa

Hili neno linatumika kuweka alama ya kutenganisha hadithi. Hapa mwandishi anasema taarifa za nyuma kuhusiana na wanafunzi kusahau kuchukua mkate.

hakuna zaidi ya mkate mmoja

Kikundi cha maneno yaliyo kinyume "hakuna zaidi" hutumiwa kusisitiza namna ya kiasi kidogo cha mkate waliokuwa nao. "mkate mmoja tu"

Kuwa macho na ujilinde

Haya maneno mawili yana maana ya kufanana na yanarudiwa hapa kwa msisitizo. Yanaweza kuanganishwa. "Kuwa macho"

chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.

Hapa Yesu anazungumza kwa wanafunzi wake katika mfano ambao hawauelewi. Yesu analinganisha mafundisho ya Mafarisayo na Herode kwa chachu, lakini hauwezi kueleza hivi unavyo tofasiri sababu wanafunzi wenyewe hawakuuelewa.