sw_tn/mat/21/15.md

1.3 KiB

Maelezo kwa ujumla

Katika mstari wa 16,Yesu anatumia nukuu toka Zaburi kuthibitisha jinsi watu walivyokuwa wamemwitikia

maajabu aliyoyataenda

"vitu vya kushangaza" au "miujiza." Hii inamaanisha Yesu alivyowaponya vipofu na vilema kati ka 21:12

Hosana

Tazama 21:9

Mwana wa Daudi

Tazama 21:9

walishikwa na hasira

Inamaanisha kuwa walishikwa na hasira kwa sababu hawakuamini kuwa Yesu ndiyo Kristo na hawakutaka watu wamsifu. "Walikasirika sana kwa sababu watu walikuwa wanamsifu"

umesikia kile kinachosemwa na hawa watu?

Wakuu wa Makuhani na waandishi wanauliza swali hili kumkemea Yesu kwa sababu wanamchukia, "Usiwaruhusu watu kusema mambo haya juu yako"

Lakini hamjawahi kusoma ... sifakamili?

Yesu anauliza swali hili kuwakumbusha wakuu wa makuhani na waandishi kile walichosoma kwenye maandiko. "Naam, nawasikia, lakini inawapasa mkumbuke mlichokisoma katika maandiko ... sifa"

Lakini hamkusoma...sifu'?

"Ndiyo nimewasikia lakini mnatakiwa kukumbuka mlichokisoma katika maandiko matakatifu...sifu'."

kutoka kwa midomo ya watoto na watoto wachanga mnayo sifa kamili

Kirai hiki "kutoka kwenye midomo" kinamaanisha kuongea. "uliwafanya watoto na watoto wachanga kusema sifa kamili"

Yesu akawaacha

"Yesu aliwaacha makuhani wakuu na waandishi"