sw_tn/mat/21/09.md

690 B

Hosana

Neno la Kiebrania linalomaanisha "Tuokoe" lakini pia linaweza kumaanisha "Kumsifu Mungu!"

Mwana wa Daudi

Yesu hakuwa mwana halisi wa Daudi, kwa hiyo hii inaweza kutafsiriwa kama "kizazi cha mfalme Daudi. Lakini pia, "Mwana wa Daudi" ni cheo cha Masihi, Huenda makutano walikuwa wakimwita Yesu kwa cheo hiki.

kwa jina la Bwana

Hapa "kwa jina la Bwana" inamaanisha "kwa nguvu ya Bwana" au "kama mwakilish wa Bwana"

Hosana juu zaidi

Neno "juu zaidi" linamaanisha Mungu atawalaye kutoka juu mbinguni. "Mungu asifiwe, ambaye yuko juu mbinguni" au "Sifa kwake Mungu"

Mji mzima ulitaharuki

Neno "mji" linamaanisha wakazi wa mji huo. "Watu wengi mjini kote walitaharuki"