sw_tn/mat/17/intro.md

796 B

Mathayo17 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Eliya

Nabii Malaki alitabiri kwamba siku moja Eliya atarudi kabla Masihi hajaja. Yesu anaelezea kwamba Yohana Mbatizaji alitimiza unabii huu kwa kumtumikia Mungu kwa namna ile ile kama Eliya. (Angalia: [[rc:///tw/dict/bible/kt/prophet]] na [[rc:///tw/dict/bible/kt/christ]])

"Yeye (Yesu) alibadilishwa"

Utukufu wa Mungu unaonekana kama mwanga mkubwa, katika maandiko. Utukufu wa Mungu daima humhofisha mtu anayeuona. Tukio hilo, lililoko katika sura hii, linaitwa "kubadilika," ambako Yesu anabadilika ili aonyeshe utukufu wake wa uungu. (Angalia: [[rc:///tw/dict/bible/kt/glory]] na [[rc:///tw/dict/bible/kt/fear]])

<< | >>