sw_tn/mat/16/intro.md

1.3 KiB

Mathayo16 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mkate

Mkate ni picha maalum katika 16:5-12. Yesu alitumia mjadala wa wanafunzi wake kuhusu mkate ili kuwaonya dhidi ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo. Aliyazungumzia mafundisho haya kana kwamba yalikuwa chachu, kiungo ambacho husababisha mkate kuinuka kabla ya kuokwa.

Wakati huo huo, kutajwa kwa mkate katika sura hii ni maana ya kuwakumbusha wasomaji kwamba Yesu alilisha watu elfu tano na mkate (tazama: Mathayo 14:13-21) na pia watu elfu nne (tazama: Mathayo 15:29-39 ). Maana ni kwamba Yesu hutoa mkate mzuri (mafundishoa), lakini Mafarisayo na Masadukayo hawafanyi hivyo.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Mathayo 16:21 huunda mkatizo katika maelezo haya. Katika hatua hii, Mathayo anatoa maoni kuhusu matendo ya Yesu ambayo yataendelea katika siku zijazo. Ni muhimu kwa mtafsiri kuashiria wazi wazi kwamba maoni haya ni kuhusu siku zijazo, yaliyoingizwa katika maelezo.

Paradox

Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Kitendawili kiko katika sura hii: "Yeyote anayetaka kuokoa maisha yake ataipoteza, na yeyote anayepoteza maisha yake kwa ajili yangu ataipata." (Mathayo 16: 24-28).

<< | >>