sw_tn/mat/11/23.md

1.8 KiB

Sentensi unganishi:

Yesu anaendelea kukemea miji ambayo miujiza yake ilitendeka karibuni.

Wewe, Kapernaum

Yesu sasa anaongea na watu wa mji wa Kapernaum kama vile walikuwa wanamsikiliza, lakini walikuwa hawasikilizi. Kiwakilishi ''wewe'' ni cha umoja kinarejelea Kapernaum kwa mistari yote miwili.

wewe

Matukio yote ya kiwakilishi cha "wewe" yakao katika umoja. Kama kinatumika kila mahali kuonyesha watu wa mji, basi kiwakilishi cha wewe kitafsiriwe katika wingi wake

Kapernaum...Sodoma

Majina ya miji hii yametumika kumaanisha watu waliokuwa wanaishi Kapernaum na Sodoma.

unadhani utainuliwa hadi mbinguni?

"unadhani utainuliwa hadi mbinguni ?" Yesu anatumia balagha kuwakemea watu wa Kapernaum kwa majivuno yao. "inaweza pia kutumika kwa mfumo tendaji. "huwezi kujiinua mwenyewe hadi mbinguni" au "sifa za watu wengine haziwezi kukuinua hadi mbinguni kama unavyodhani atafanya"

utashuswa hadi chini kuzimu

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji ''Mungu atakupeleka hadi kuzimu.''

Kama katika Sodoma ... ingekuwepe hadi leo

Yesu anatumia mazingira ya kubuni ambayo yangetokea katika siku zilizopita, lakini haikutokea.

matendo makuu

''''matendo makuu'' au ''kazi ya nguvu za Mungu'' au "miujiza"

ingekuwepo hadi leo

Kiwakilishi ''inge'' kinarejelea kwa mji wa Sodoma

nasema kwako

Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye

itakuwa rahisi kwa nchi ya Sodoa kusimama katika siku ya hukumu kuliko wewe

Hapa "nchi ya Sodoma" inamaansha watu walioishi kule. ''Mungu ataonyesha rehema kwa watu wa Sodoma katika siku ya hukumu kuliko kwako'' au Mungu atawapa adhabu kali zaidi katika siku ya hukumu kuliko watu wa Sodoma.''

kuliko wewe

Taarifa zilizofumbwa ziwekwe wazi. "kwa sababu haukutubu na kuniamini, ingawa uliniona nikifanya miujiza"