sw_tn/mat/05/intro.md

1.0 KiB

Mathayo 05 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Mathayo 5-7, ambayo huitwa "Mahubiri ya Mlimani," ni funzo moja ndefu ya Yesu. Mgawanyiko wa sura husababisha kuchanganyikiwa hapa. Kichwa kinaweza kumsaidia msomaji kuelewa kwamba sura hizi zinaunda sehemu moja au kitengo. Mtafsiri anapaswa kufahamu kuwa kuna swali fulani kuhusu ikiwa mafundisho yanahusu Israeli, kanisa, au ufalme wa Mungu wa baadaye.

5:3-10, inayojulikana kama Heri au Baraka, imewekwa kwa kutumia uingizaji, na kila mstari unaanza na neno "heri." Uingizaji huu unaashiria fomu ya ushairi wa mafundisho haya.

Dhana maalum katika sura hii

"Wanafunzi wake"

Inawezekana kutaja mtu yeyote aliyemfuata Yesu kama mfuasi au mwanafunzi. Yesu aliwachagua wafuasi wake kumi na wawili kuwa watu wake wa ndani, wale wanafunzi kumi na wawili. Baadaye walijulikana kama mitume. Inaweza kuwa na maana kwamba mafundisho haya yalikuwa kwa mitume hao kumi na wawili.

<< | >>