sw_tn/mat/05/29.md

1.4 KiB

Na kama ... lako

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye kwa mtu binafsi Matukio yote ya viwakilishi vya "ku" na "lako" viko katika umoja, lakini unaweza kuvitafsiri katika wingi.

kama jicho lako la kulia linakusababisha kujikwaa

Hapa "jicho" linamaanisha kile ambacho mtu hukiona. Na "kujikwaa". Ni sitiari ya "dhambi." "Kama kile ukionacho hukusababisha kujikwaa" au "kama unataka kufanya dhambi kwa sababu ya kile ukionacho"

jicho lako la kulia ... mkono wako wa kuume

Hii inamaanisha jicho au mkono ule wa muhimu zaidi, dhidi ya mkono au jicho la kushoto. Hapa unaweza kutafsri "kulia" kuwa "ndiyo nzuri zaidi" au "kulia pekee."

ling'oe

"litoe kwa nguvu" au "liharibu" kama jicho lako la kulia halijatajwa rasmi, unaweza kuitafsiri hii kama " kuharibu macho yako." kama macho yametajwa, unaweza kuyatafsiri kama "yaharibu"

ling'oe ... likate

Yesu analikuza zaidi jambo hili juu ya jinsi ambavyo mtu anapaswa kuiona jinsi dhambi ilivyo mbaya kulichukulia kwa umakini swala hili.

uutuplie mbali na wewe

"achana nao"

kiungo kimoja katika mwili wako kiharibike

"upoteze sehemu ya mwili wako"

kuliko mwili mzima kutupwa jehanamu

Hili linaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "kuliko Mungu kuutupa mwili wako wote jehanamu"

kama mkono wako wa kuume unakusababisha

katika hii lugha ya umbo, mkono unasimama badala ya matendo la mwili wote