sw_tn/mat/01/22.md

814 B

Taarifa kwa ujumla

Mwandishi amnukuu nabii Isaya kuonesha kwamba kuzaliwakwa Yesu kulikuwa kwa mujibu wa andiko

Hii yote ilitokea

Malaika hazungumzi tena. Mathayo sasa anaeleza umuhimu wa kile malaika alikisema.

kilichonenwa na Bwana kwa njia ya nabii

Hii inaweza kuelezwa kwa namna iliyo tendaji. "kile ambacho Bwana alimwambia nabii Isaya kuandika zamani."

Tazama...Emanueli

Hapa Mathayo anamnukuu nabii Isaya.

Tazama

Neno hili huongeza msisitizo kwa kile kilicho fuata kusemwa. "Tazama" au "Sikia" au "Kuwa makini kwa kile ninachotaka kukuambia"

Emanueli

Hili ni jina la kiume.

maana yake 'Mungu pamoja nasi'

Hii haimo katika kitabu cha Isaya. Mathayo anaeleza maana ya jina "Emanueli." Unaweza kulitafsiri kama sentenso iliyo peke yake. "Jina hili maana yake 'Mungu pamoja nasi.'"