sw_tn/job/42/01.md

735 B

"Ninajua kwamba unaweza kufanya mambo yote, ya kuwa hakuna kusudi lako linaweza kuzuiliwa.

"Ninajua kwamba wewe unaweza kufanya mambo yote. Ninajua kwamba hakuna kusudi lako lolote linaweza kuzuiliwa." Hili ni wazo lile lile limeelezwa kwa jinsi mbili tofauti.

hakuna kusudi lako linaweza kuzuiliwa

"hakuna yeyote awezaye kuzuia kusudi lako lolote"

Ni nani huyo ambaye pasipo maarifa huificha mipango?

Matoleo mengi ya kisasa hukubaliano kwamba Ayubu ananukuru maneno ya Mungu kutoka katika 38:1. Wafasiri wanaweza kuamua kuiweka wazi kwamba Mungu alimwuliza swali hili Ayubu, na ya kwamba Ayubu kwa sasa analikumbuka.

huificha mipango

Hii ina maana kwamba, kuficha au kutoiwakilisha mipango ya Mungu na ushauri wake.