sw_tn/job/21/16.md

1.2 KiB

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Tazama, je kufanikwa kwao hakupo mikono mwao mwenyewe?

hapa "mikono" inamaanisha nguvu zao au utawala wao. Ayubu anatumia swali hili kutoa changamoto kwa rafiki zake. KT: "Tazama, watu hawa waovu wanasema kwamba wamesababisha mafaniki wao wenyewe!"

Je ni mara ngapi... msiba wao huwajilia?

Ayubu anatumia swali hili kusisitiza kuwa yeye anaona kwamba Mungu hawaadhibu waovu mara nyingi. KT: "si mara nyingi ... msiba wao huwapata "

taa ya watu waovu imezimwa

Ayubu analinganisha kuzima taa na kufa. KTN: "Mungu husababisha wafe ghafla"

Ni mara ngapi hutokea... katika hasira yake?

Ayubu anatumia swali hili la pili kuweka mkazo kuwa inaonekana mara nyingi Mungu huwa hawaadhibu waovu. KTN: "Si mara nyingi ... katika hasira yake."

Ni mara ngapi ... dhoruba huwabeba?

Ayubu anatumia swali hili la tatu kuweka mkazo kuwa inaonekana mara nyingi Mungu huwa hawaadhibu waovu.KTN: "Si mara nyingi ... dhoruba huwabeba."

wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi ambayo huchukuliwa na dhoruba

Kifo cha waovu kinaongelewa kana kwamba ni makapi yasiyofaa na mabua yapeperushwayo.KTN: "Mungu huwaondoa kama upepo upeperushao makapi"