sw_tn/job/21/07.md

841 B

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Kwa nini watu waovu wanaendelea kuishi na kuwa wazee na kustawi katika nguvu nyingi?

Ayabu anatumia swali hili kuonesha kuwa rafiki zake walikosea kudhani kwamba watu waovu mara nyingi hupatwa na mateso. KN: " watu waovu huendelea kuishi, huzeeka, na kuwa na utajiri zaidi"

Wazao wao huimarika pamoja nao katika upeo wao...kizazi chao mbele ya macho yao.

Vishazi hivi viwili vinamaana ya jambo moja na vinaweka msisitizo kuwa jambo hili ni la kweli.

katika upeo wao... mbele ya macho yao

Misemo hii inamaanisha jambo moja kwa sababu "macho" yanahusiana na upeo wa kuona. Watu waovu huwaona wazoa wao wakistawi na kutajirika.

Nyumba zao

Hapa "nyumba" inamaanisha wanafamilia wanaoishi humo. KT: "Familia zao"

fimbo ya Mungu

inamaanisha adhabu ya Mungu.