sw_tn/job/20/10.md

799 B

Habari za Jumla:

Sofari anaendelea kuzungumza kwa Ayubu.

Watoto wake

"Watoto wa mtu mwovu"

mikono yake itaweza kurudisha utajiri wake.

Katika sentensi hii "mikono"inamaanisha watoto wa mtu mpumbavu. Wakati atakapokufa watoto wake watapaswa kurudisha kila kitu ambacho yeye alikichukua kwa watu wengine.

Mifupa yake imejaa nguvu za ujanani,

"Mifupa" yake inawakilisha mwili wake. Kuwa "umejawa" na nguvu za ujanani kunawakilisha kuwa na nguvu kama mtu kijana."Mwili wake una nguvu kama mwili wa mtu kijana"

lakini zitalala naye chini katika mavumbi.

Sentensi hii inamaanisha nguvu zake za ujanani "kulala chini katika mavumbi" kunawakilisha kupotelea mbali. " lakini nguvu zake za ujanani zitakufa maoja naye" au "lakini nguvu zake za ujanani hazitaonekana wakati atakapokufa"