sw_tn/job/16/06.md

1.2 KiB

kuomboleza

Ayubu amepitia majonzi mazito ya kupoteza familia yake na afya hiyo ni haielezeki na kwa hiyo, inamsababishia yeye "huzuni kubwa na maumivu ya hisia."

jinsi gani mimi ninasaidiwa?

Ayubu anatumia swali hili la kizushi kueleza kuwa kunyamaza kimya hakupunguzi huzuni yake yeye. Swali hili laweza kuandikwa bila kuwekwa katika hali ya swali. "hainisaidii mimi hata kidogo."

Lakini sasa, Mungu wewe

Ayubu sasa anarudisha lalamiko lake kwa Mungu.

umeifanya familia yangu yote kuwa ukiwa.

"umeharibu familia yangu yote"

Wewe umenifanya mimi kukauka,

Sentensi hii inamaanisha kuwa mwili wa Ayubu umekonda na kuwa na mikunjamano. "Wewe umeufanya mwili wangu kukonda"

ambayo yenyewe ni ushuhuda dhidi yangu mimi

Ayubu anaelezea kukonda kwa mwili wake kama vile ulikuwa kama mshitaki dhidi yake "na watu wanafikiri kuwa unanionyesha mimi kuwa ni mwenye dhambi"

kukonda kwa mwili wangu huinuka dhidi yangu, na kunashuhudia dhidi

Ayubu anaelezea hali ya kukonda kwa mwili wake kama vile ulikuwa mshitaki dhidi yake yeye. "Wote wanaona jinsi mwili wangu ulivyokonda, na wanafikiri hicho kinathibitisha kuwa mimi ni mwenye hatia"

dhidi ya macho yangu.

Hapa Ayubu anazungumzia kwa "uso "wake. "dhidi yangu mimi"