sw_tn/job/15/01.md

976 B

Elifazi Mtemani

Hili ni jina la mtu. Watu kutoka temani wanajulikana kama Watemani.

Mtu mwenye hekima anapaswa kujibu kwa maarifa yasiyofaa na kujijaza mwenyewe na upepo wa mashariki?

Elifazi anatumia swali hili la kejeli kumkemea Ayubu. "Mtu mwenye busara hapaswi kujibu kwa maarifa yasiyo na faida wala kujilisha yeye mwenyewe na upepo wa mashariki"

kujijaza mwenyewe na upepo wa mashariki?

Upepo unawakilisha hakuna. Tungo hii inazungumzia mtu anyezungumza maneno yasiyo na maana.Mtu huyu ni kama amejaa upepo. "kujijaza yeye mwenyewe na maneno yasiyo na maana"

upepo wa mashariki?

"upepo wa joto" au "upepo wa jangwani"

Anapaswa kuhojiana na mazungumzo yasiyo na faida au na hotuba ambazo kwa hizo yeye hawezi kufanya mema?

Elifazi anatumia swali hili la kizushi kumkemea Ayubu. " Yeye hapaswi kuhojiana na kwa mazungumzo yasiyo na faida" au "Yeye hapaswi kushindana kwa kutumia maneno yasiyo na faida au kutoa hotuba ambazo mwisho wake ni hasara"