sw_tn/job/10/10.md

1020 B

Habari za Jumla:

Katika mistari hii, Ayubu anatumia lugha ya ushairi kuelezea namna Mungu alivyo muumba yeye katika tumbo la uzazi.

Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?

Hili ni swali ambalo linatarajia jibu halisi. "Wewe ulinimimina kama maziwa na kunigandisha kama jibini." au "Wewe umenitengeneza mimi katika tumbo la uzazi kama maziwa yamiminavyo na kuwa jibini."

Wewe

Hapa "wewe" linahusiana na Mungu.

mimi

Hapa "mimi" linahusiana na Ayubu.

Umenivika ngozi na nyama

Mungu kuweka ngozi na nyama juu ya mwili wa Ayubu inaongelewa kana kwamba Mungu alimvisha nguo yeye. "Wewe umeweka ngozi na nyama juu ya mwili wangu"

niunganisha pamoja

"umenifuma." Mungu anaunganisha mwili wa Ayubu katika tumbo la uzazi inaongelewa kana kwamba Mungu alikuwa anafuma au anashona kipande cha nguo."niunganishe"

misuri

"mikano." Hizi ni sehemu za mwili ambazo huunganisha misuli na mifupa au sehemu zingine za mwili na ziko kama kwamba ni ngumu, utepe mweupu au kamba nyembamba.