sw_tn/job/06/14.md

992 B

Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake

"Rafiki anatakiwa kuwa na huruma kwa mtu ambaye anajihisi kukata tamaa"

hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi

"hata kama ataacha kumweshimu Mwenyezi Mungu" Maana za kufaa ni 1) mtu hana hofu ya Mungu au 2) rafiki zake hawamwogopi Mungu.

Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani

Ayubu anawaelezea rafiki zake kuwa wamekuwa kama "bondejangwa" ambalo hupitiwa na mto katikati yake ambao unaweza kukauka ghafra na si wa kutumainika.

mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu

"mfano wa mito ya maji ambayo hukauka"

ambayo imetiwa giza kwa sababu ya barafu juu yake

"ambayo ni giza kama barafu"

na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake

"na theluji hujificha ndani yake" au "barafu hupotea ndani yake"

Wakati zikiyeyuka, hutoweka

"Wakati zikipata joto, hutoweka"

kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.

"wakati wa joto, hukauka"