sw_tn/job/04/07.md

1.6 KiB

ni nani aliyeangamia akiwa hana kosa?

Elifazi anatumia swali hili kumshawishi Ayubu kuchunguza dhambi katika maisha yake (na hukumu takatifu ya Mungu) kama kisababishi cha yeye kupotea. "Hapa mmoja aliyeangamizwa wakati hana kosa."

ni lini watu wakamilifu walikatiliwa mbali

Swali hili pia linamaanisha kutengeneza maelezo, na yanaweza kuwekwa katika umbo la kufaa. "Hakuna hata mmoja aliyewahi kumkatilia mbali mtu mkamilifu."

katiliwa mbali

Hapa kukatiliwa mbali inamaanisha kuangamizwa.

walimao uovu ... kupanda taabu ... huvuna

Hapa matendo ya kulima na kupanda yanawakilisha kinacho sababisha taabu kwa watu wengine. Tendo la kuvuna ni mfano wa mateso ya taabu ambazo mtu huzisababisha mwenyewe.

Kwa pumzi ya Mungu huangamia; kwa mlipuko wa hasira zake huteketea

Mwandishi anaeleza wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti. Huu ni muundo wa ushairi wa kiebrania utumikao kwa kusisitiza, udhahiri, mafundisho, au yote matatu.

pumzi ya Mungu

Hii inaweza kuwa mfano wa tendo la Mungu la kutoa amri.

mlipuko wa hasira

Usemi huu unaashiria upumuaji mkubwa ambao mtu wakati fulani huufanya kupitia pua zake wakati akiwa na hasira.

pumzi ... mlipuko

msemo wa pili umejengwa juu ya wa kwanza. Zinaunda wazo moja kwa kutumia maana ambazo zinaongeza matokeo. "Kwa mpumuo wa mdomo wa Mungu wanafariki; mwendo kasi wa upepo wa hasira zake huwateketeza wao."

huangamia ... huteketea.

Fungu la pili limejengwa juu ya la pili. Yanaunda wazo moja. "Kwa mpumuo wa mdomo wa Mungu wanafariki; mwendo kasi wa upepo wa hasira zake huwateketeza wao."

huteketea.

Hapa kuteketezwa au kuliwa ni mfano wa kuuliwa.