sw_tn/jas/05/07.md

772 B

Sentensi unganishi

Yakobo anabadilisha mada toka kwenye kuwakemea matajiri na kuwapa mawaidha waamini.

Maelezo ya jumla

Kwa kufunga Yakobo anawakumbusha waamini kuhusu ujio wa Bwana na kuwapa mafundisho mafupi namna ya kuishi kwa ajili ya Mungu.

Kwa hiyo vumilieni

"Kwa ajili ya hili kuweni na subira na uvumilivu"

mpaka ujio wa Bwana

Sentensi hii inaelezea ujio wa Yesu, atakapoanzisha ufalme wake duniani na kuhukumu watu wote. "Mpaka Kristo atakapokuja"

Mkulima

Katika mazungumzo haya Yakobo anatumia mkulima na mwamini kuelezea namna ya kuwa mvumilivu.

Kazeni mioyo yenu

Yakobo anawataka waamini wawe na mioyo thabiti na kuwa na msimamo. "Kuweni na msimamo" au "Ifanyeni imara mioyo yenu"

kuja kwake Bwana ni karibu.

"Bwana atarudi mapema"