sw_tn/jas/05/04.md

1.3 KiB

Sentensi unganishi

Yakobo anaendelea kuwaonya matajiri juu ya starehe na utajiri.

malipo ya watendakazi-wale ambao hamjawalipa kwa kuvuna katika mashamba yenu- wanalia

Pesa ambayo ilitakiwa ilipwe imeelezewa hapa kama mtu anayelalamika juu ya dhuluma aliyofanyiwa. "kwa kuwa hamwalipi mliowaajiri kufanya kazi kwenye mashamba yenu mnafanya makosa"

kilio cha wale waliovuna mazao yenu kimeyafikia masikio ya Bwana wa Majeshi.

Kilio cha wanaovuna kimesikika mbinguni. "Bwana wa majeshi amesikia kilio cha wavunaji"

kwenye masikio ya Bwana wa Majeshi

Mungu anazungumziwa kuwa ana masikio kama mwanadamu. "Bwana wa majeshi amesikia"

Mmejinenepesha mioyo yenu kwa siku ya machinjo

Hapa watu wanaelezewa kama wanyama, wanaolishwa vizuri ili wanenepe na kuchinjwa kwa ajili ya karamu. Japokuwa hamna atakayesherehekea siku ya hukumu. "Tamaa zeni zinawaandaa kwa hukumu ya milele"

mioyo yenu

"Mioyo" imezungumziwa kama kituo cha tamaa za mwanadamu. Neno hili linasimama kumuelezea mtu kwa ujumla.

Mmemhukumu ... mwenye haki

"Mmehukumu" inaweza isiwe na maana ya kisheria ya kupitisha hukumu ya kifo. Bali inawazungumzia watu waovu na wenye nguvu wanaoamua kuwanyanyasa masikini mpaka wanakufa.

mwenye haki

"Mtu anayefanya mambo yanayofaa" Hii sentensi inaelezea watu wenye haki kwa ujumla na sio mtu mmoja.

asiyeweza kuwapinga

"Asiye kinyume na ninyi"