sw_tn/jas/02/14.md

1.2 KiB

Sentensi unganishi

Yakobo anawatia moyo waamini waliotawanyika kuonyesha imani yao mbele za watu. Kama vile Abrahamu alivyoionesha imani yake kwa vitendo.

Kuna uzuri gani, ndugu zangu, kama mtu anasema ninayo imani, lakini hana matendo?

Yakobo anatumia swali kuifundisha hadhira yake. "Waamini wenzanhu, sio vizuri kabisa mtu akisema ana imani lakini hana matendo."

anayo imani

Yakobo anazungumzia imani, kumuamini Mungu.

haina matendo

Yakobo anazungumzia matendo kuwa ni kufanya matendo mema.

Je, imani hiyo yaweza kumwokoa?

Yakobo anazungumzia imani kuwa kumuamini Mungu kuna nguvu ya pekee katika kumuokoa mwanadamu lakini Imani haitoshi. "Imani hiyo haiwezi kumuokoa."

kumuokoa

"Kumuokoa toka kwenye hukumu ya Mungu."

mkaote moto

"kuwa na nguo za kutosha kuvaa" au "kuwa na sehemu ya kulala."

mle vizuri

"kuwa na chakula cha kutosha."

ya mwili

kula, kuvaa na kuishi vizuri.

yafaa nini?

Yakobo anatumia swali hili kuifundisha hadhira. "hivi sio vizuri."

wa kiume na wa kike

Waamini wenzangu katika Yesu, wanaume kwa wanawake

imani ... imekufa

Yakobo anaizungumzia imani kuwa ni hai mtu afanyapo matendo mema na imekufa kama mtu hatafanya matendo mema.

imani ... ina matendo

Imani inaambatana na mtu afanyaye matendo mema.