sw_tn/jas/01/22.md

901 B

Litiini neno

Wanapaswa kutii amri zilizoamriwa na Mungu.

Mkijidanganya wenyewe

"mnajidanganya wenyewe

Kwa kuwa kama yeyote alisikiaye neno bila kulitendea kazi ni sawa na mtu ajiangaliaye uso wake halisi katika kioo.

Mtu anayesikiliza maneno ya Mungu lakini hayatii anafananishwa na mtu anayejiangalia kwenye kioo na baadae anasahau muonekano wake.

uso wake halisi

Uso wake kama ulivyo.

Hujitathmini uso wake na baada ya mda mfupi husahau

Mtu anayejiangalia uso wake na baadae akasahau muonekano wake ni sawa na mtu aliyesikia neno la Mungu na kusahau alichosikia.

mtu yule anayeiangalia kwa uangalifu sheria kamili.

Hii inaendelea kuelezea picha ya sheria kama kioo.

Sheria kamili ya uhuru

"sheria kamili inayoruhusu watu kuwa huru"

Mtu huyu atabarikiwa katika utendaji wake.

Hii inaweza kuelezewa katika hali ya kutenda "Mungu atambariki huyu mtu kama akiitii sheria"