sw_tn/jas/01/17.md

957 B

Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika

Sentensi hizi mbili zina maana moja. Yakobo alizitumia kusisitiza kuwa kila kizuri alichonacho mtu kinatoka kwa Mungu.

Baba wa nuru.

Mungu, muumbaji wa nuru zote zilizopo juu angani (jua, mwezi na nyota) inajulikana kuwa ni Baba yao.

Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo

Hii inamuelezea Mungu kama mwanga usiobadilika tofauti na jua, mwezi, sayari na nyota ambazo zinapita katikati ya anga na zinabadilisha nuru yake. "Mungu habadiliki kama jua, mwezi na nyota ambazo zinatokea na kupotea"

Kutupa sisi

Neno "sisi" linamaanisha Yakobo na hadhira yake.

Katupa uzima

Mungu aliyetupa uzima wa milele anazungumziwa kana kwamba ametupa uzima.

Neno la kweli

Ujumbe wa kweli wa Mungu.

Kama uzao wa kwanza

Yakobo anatumia utamaduni wa Kiebrania wa zao la kwanza kama njia ya kuelezea thamani ya Mwamini wa Kikristo kwa Mungu. anaelezea kuwa kutakuwa na waamini wengi sana baadae.