sw_tn/jas/01/17.md

28 lines
957 B
Markdown
Raw Permalink Normal View History

2018-04-12 01:01:04 +00:00
# Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika
Sentensi hizi mbili zina maana moja. Yakobo alizitumia kusisitiza kuwa kila kizuri alichonacho mtu kinatoka kwa Mungu.
# Baba wa nuru.
Mungu, muumbaji wa nuru zote zilizopo juu angani (jua, mwezi na nyota) inajulikana kuwa ni Baba yao.
# Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo
Hii inamuelezea Mungu kama mwanga usiobadilika tofauti na jua, mwezi, sayari na nyota ambazo zinapita katikati ya anga na zinabadilisha nuru yake. "Mungu habadiliki kama jua, mwezi na nyota ambazo zinatokea na kupotea"
# Kutupa sisi
Neno "sisi" linamaanisha Yakobo na hadhira yake.
# Katupa uzima
Mungu aliyetupa uzima wa milele anazungumziwa kana kwamba ametupa uzima.
# Neno la kweli
Ujumbe wa kweli wa Mungu.
# Kama uzao wa kwanza
Yakobo anatumia utamaduni wa Kiebrania wa zao la kwanza kama njia ya kuelezea thamani ya Mwamini wa Kikristo kwa Mungu. anaelezea kuwa kutakuwa na waamini wengi sana baadae.