sw_tn/isa/57/03.md

1008 B

Lakini njooni hapa

Mungu anawaita watu wote ambao sio waaminifu kuja mbele yake ili awahukumu katika utofauti mkubwa kwa ahadi kwa ajili ya wenye haki waliotangulia.

wana wa mwanamke mchawi

Hii ni fedheha kubwa dhidi ya watu ambao hufanya uchawi kwa sababu uchawi na mazingombwe hujumuisha kuabudu sanamu.

watoto wa mzinzi na mwanamke ambaye amejifanya kuwa kahaba

Hii ina maana ya uzinzi halisia na wa kiroho. Wamemuacha kuabudu Mungu na sasa wanaabudu miungu mingine pamoja na ukahaba halisia katika sherehe za Wakaanani.

Ni nani ambaye unafurahia kumdhihaki? Ni dhidi ya nani unafungua mdomo na kuchomoza ulimi wako?

Yahwe anatumia maswali kukaripia watu ambao wanamdhihaki kupitia kuabudu kwa uongo. "Mnanidhihaki na kunikejeli kwa kufungua mdomo wako wazi na kuchomoza nje ulimi!"

Je! wewe siye watoto wa uasi, watoto wa udanganyifu?

Yahwe anatumia swali lingine kukaripia watu. Hii haimanshi kuzaliwa kwao lakini hali yao ya kiroho. "Nyie ni watoto wa uasi, watoto waa udanganyifu!"