sw_tn/isa/53/08.md

1.2 KiB

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kumfafanua mtumishi wa Yahwe.

Kwa kuonewa na kuhumiwa alishutumiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Walimtendea kwa ukatili, wakamhukumu, na wakamshutumu"

kuonewa

Neno la Kiebrania linatafsiriiwa hapa kama "kuonewa" na baadhi ya tafsiri kama "kukamata". Kwa tafsiri hizi, wazo ni kuwa Mtumishii atakamatwa na kisha kuhukumiwa na kushutumiwa.

nani kutoka kizazi hicho alimfikiria tena juu yake?

Swali hili linasisitiza ya kwamba hakuna mtu anayemfikiria. "hakuna mtu kutoka kizazii chake aliyejali nini kilitokea kwake" au "hakuna mtu kati ya walioishi naye walijali nini kilitokea kwake"

nani kutoka kizazi hicho alimfikiria tena juu yake?

Tafsiri nyingi zinatafsiri sehemu hii kwa Kiebrania tofauti. "Nani anaweza kusema jambo juu ya uzao wake? au "Nani anaweza kusema kitu kuhusu hatma yake?"

lakini aliondolewa kutoka katika nchi ya walio hai

"Kuondolewa" hapa ina maana ya kifo. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Lakini alikufa" au "Lakini kifo kikamchukua"

ya watu wangu

"ya watu wa Israeli"

wala hapakuwa na udanganyifu katika kinywa chake

"Kinywa" inawakilisha kile mtu anachosema. "wala hakumdanganya yeyote alipozungumza"